Wakurugenzi Watendaji SIMIYU Waagizwa Kulipa Stahiki za Madiwani


Na. Mwandishi Wetu, SIMIYU

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka amewaagiza Wakurugenzi watendaji wa Halmashauri zote sita mkoani humo, kuhakikisha wanalipa stahiki za madiwani kabla ya mabaraza ya madiwani kuvunjwa wiki tatu zijazo.

Mkuu huyo wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka, ametoa agizo hilo katika baraza maalumu la madiwa wa Halmasahauri ya Wilaya ya Busega, kwa ajili ya kujadili hoja za mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali CAG.

Katika hatua nyinge, Mtaka ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Busega kuweka mkazo katika ukusanyaji mapato, kutokana na kukusanya chini ya kiwango, ambapo kwa sasa inakusanya asilimia 45 pekee.

Kauli hiyo imeungwa mkono na Madiwani wa Halmashauri hiyo, wakisema pamoja na kupata hati safii, suala la kuongeza ukusanyaji mapato ni muhimu ili Halmashauri iweze kujiendesha na kuhudumia wananchi.

Kwa upande wake Mbunge wa Busega, Dkt. Raphael Chegeni, amesema ukusanyaji mapato ni muhimu, hasa ikizingatiwa kwamba bado kunahitajika ujenzi wa miundombinu ya madarasa ili kutosheleza mahitaji ya wanafunzi hususan wanaojiunga na elimu ya sekondari.

MWISHO

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.