Wakulima Mahiri Kuanza Kupimwa kwa Sifa

Na. Amiri Kilagalila, NJOMBE
Kutokana na kuongezeka kwa idadi ya wakulima inayopelekea kukuwa kwa sekta ya kilimo na kusaidia kuongezeka kwa pato la mkulima na Taifa, kituo cha utafiti wa kilimo (TARI) Uyole, wanasema lengo la kituo kwa sasa ni kuona mkulima mahiri na anayefanikiwa katika maisha kutokana na kilimo bora na chenye tija.

Amebainisha hilo Dkt. Tulole Lugendo Bucheyeki mkurugenzi wa kituo cha TARI Uyole,wakati akikagua maendeleo ya shamba la mkulima wa Mahindi kupitia mradi wa kuboresha kilimo na maisha ya mkulima kwa kutumia mbegu bora lililopo kijiji cha Ilunda kata ya Mtwango wilayani Njombe.

Vilevile, amesema kwa sasa kituo cha Uyole kina aina zaidi ya 8 ya Mahindi zitakazomuwezesha mkulima wa sehemu mbali mbali nchini kufaidika yatakapotunzwa,huku akibainisha kuwa awali walikuwa na  mbegu kwa ajili Nyanda za juu kusini tofauti na sasa.

Lornad Sabula ni mtafiti kutoka taasisi ya utafiti wa kilimo Tanzania kituo cha Uyole na meneja wa mradi wa Pata Tija,anasema kwa sasa wanahitaji kubadilisha mtazamo wa kilimo kwa wakulima zaidi ya laki moja katika mazao ya Mahindi, Maharage na Soya.

Jafari Mbogela na Anna Wikichi ni wakulima wa kijiji cha Ilunda wanasema wamepata mafanikio makubwa katika kilimo kutokana na matumizi ya Mbegu bora za kilimo kutoka kituo cha utafiti TARI, hali ambayo imewawezesha kupata zaidi ya gunia 50 za mahindi kwa ekari moja tofauti na awali.

Mpaka sasa mradi wa kuboresha kilimo na maisha ya wakulima umefanikiwa kuwafika wakulima elfu hamsini wa moja kwa moja katika mikoa ya nyanda za juu kusini, huku wengine wakifikiwa kupitia kwa wagani, maonyesho ya kilimo pamoja vyombo vya Habari.


MWISHO

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.