Na. Jonas Kamaleki, DODOMA
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli
ameiagiza Wizara ya Fedha na Mipango kutoa Shilingi bilioni 2 kwa ajili ya
kukamilishaujenzi wa Ofisi ya Ikulu, Chamwino, Dodoma.
![]() |
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza wakati wa hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi mradi wa ujenzi wa Ofisi za Ikulu Chamwino Dodoma leo Mei 30, 2020 |
Rais Magufuli ametoa agizo hilo wakati wa hafla ya uwekaji wa jiwe
la msingi kwa ajili ya ujenzi wa Ikulu, iliyofanyika leo Chamwino, Dodoma.
Akionyesha kuridhishwa na kazi
inayofanywa na SUMA JKT Rais Magufuli amesema kuwa vijana 2400 wanoshiriki
ujenzi huo atawafikiria ujenzi utakapokamilika.
Rais alisema kuwa kila kazi anayowapa JKT ana uhakika wanaifanya
vizuri akitaja baadhi kama ujenzi wa ukuta wa Mirerani, mji wa Serikali, Dodoma
na kushiriki katika misheni mbalimbali za kulinda amani ndani nan je ya nchi.
“Kweli JKT mnastahili sifa mara 100 kutokana na kazi nzuri
mnayofanya, hongereni sana”, alisema Rais Magufuli.
Aidha, amewapongeza watangulizi wake
kwa hatua mbalimbali walizochukua kutimiza ndoto ya Baba wa Taifa ya kufanya
Dodoma kuwa Makao Makuu ya nchi.
“Kwa kweli Nyerere aliona mbali, tangu nihamie Dodoma, nimepapenda
sana, ni pazuri” alisisitiza Rais Magufuli na kuonyesha kuwa eneo la Chamwino
lina mandhari ya kuvutia.
Dkt. Magufuli ameongeza kuwa pamoja na
ujenzi unaoendelea, tayari majengo matatu ya awali na ujenzi wa ukuta
unaozunguka Ikulu vimeshakamilika. Aidha, hakuna jengo hata moja la zamani
litakalobomolewa.
Kwa upande wake, Rais wa Awamu ya Pili, Mhe. Ali Hassan Mwinyi
amemshukuru Rais Magufuli kwa uamzi wake wa kuhamishia Serikali Dodoma. Aidha,
amemuelezea Rais Magufuli kuwa ni mchapakazi na mbunifu.
Mhe. Benjamin William
Mkapa, Rais wa Awamu ya Tatu amesema kuwa uamzi wa Serikali kuhamia Dodoma ni
jitihada za muda mrefu na kila awamu ilifanya jitihada, Rais Magufuli amefanya
mengi zaidi na sasa Serikali imehamia Dodoma.
![]() |
Rais wa Awamu ya Tatu Mhe. Benjamin Mkapa akizungumza wakati wa hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi mradi wa ujenzi wa Ofisi za Ikulu Chamwino Dodoma leo Mei 30,2020 |
Akitoa salamu kati
hafla hiyo, Rais wa Awamu ya Nne, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amempongeza
Rais Magufuli kwa uamzi wa busara na wa hekima wa kujenga Ikulu, na
kuongeza kuwa hapo ndio kilele chenyewe.
![]() |
Rais wa Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza wakati wa hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi mradi wa ujenzi wa Ofisi za Ikulu Chamwino Dodoma leo Mei 30,2020 |
Chanzo:
Maelezo Blog
Comments
Post a Comment