Waziri Jafo Awataka Wanafunzi Kuzingatia Masomo

Na. Mwandishi Wetu, DODOMA

WAZIRI wa Nchi,
Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Selemani Jafo amelitaka Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA) na Taasisi ya elimu (TET) kuhakikisha utaratibu wa kufanya marejeo ulioanza kwa kidato cha sita uhusishe madarasa yote yanayotarajia kufanya mitihani ya Taifa.

Aidha, amewataka wanafunzi kuzingatia ratiba ya masomo inayotolewa ili wasikose vipindi na hivyo kuwafanya kuwa nyuma tofauti na wenzao pindi wakirudi shuleni.

Waziri Jafo ametoa maelekezo hayo leo ofisini kwake wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu utaratibu wa masomo kwa njia ya runinga,redio na mitandao ya kijamii.

AMEzipongeza taasisi zote binafsi zilizoshirikiana na serikali kuhakikisha lengo lake linatimia katika kipindi hiki cha mpito cha ugonjwa wa Corona unaosababisha homa kali ya mapafu(COVID 19).

Akizungumzia suala la Covid 19, Waziri Jafo amependekeza kuwepo kwa wiki ya kujifukuza nchini ili kuweza kupunguza maambukizi hayo na kufuata ushauri mbalimbali unaotolewa.

Amewataka watu kutoona aibu bali wajifukize na kula lishe nzuri ili kuimarisha afya zao.


MWISHO

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.