Wajasiriamali jijini Dodoma waelezea hali ya biashara zao katika kipindi hiki cha Mlipuko wa Ugonjwa wa Corona


Na. Jackline Kuwanda, DODOMA

Licha ya uwepo wa ugonjwa wa homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona (COVID-19) hapa nchini, Wajasirimali wanaojishughulisha na shughuli mbalimbali hapa jijini Dodoma wameendelea kufanya shughuli zao kama kawaida huku wakiendelea kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa huo kwa kufuata maelekezo yote ambayo yametolewa na wizara ya Afya.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti na Mtandao wa Dodoma News Blog wajasirimali hao akiwemo Emmanuel Mazengo na Juma Athumani ambao ni wapiga picha katika bustani ya Nyerere Square wamesema kuwa uwepo wa ugonjwa huo katika biashara yao imewaathiri kwa kiasi kikubwa kwani idadi ya wateja waliokuwa wakifika katika eneo hilo imepungua tofauti na ilivyokuwa hapo awali huku wengine wakisema kuwa wanaendelea kuchukua tahadhari kama kawaida dhidi ya ugonjwa huo.

Hali ya uchumi imekuwa ngumu kwa wapiga picha na sisi tu peke yetu bali hata sekta nyingine, kwasasa unaweza kushinda bila hata kupiga picha moja, tunaona namna ambavyo vijana wetu wanahangaika hapa, sisi pia tunavyo hangaika hakuna chochote kwa upande wetu hili janga ni kubwa’’.

Ally Gwendo ni Mjasirimali anayejishughulisha na bidhaa za uchongaji wa vinyago yeye anasema kwa sasa kwa wachonga vinyago hali imekuwa si nzuri ambapo kwa  pindi cha nyuma hali ya wateja ilikuwa ni kubwa lakini kwa sasa upatikanaji wa wateja umekuwa ni mgumu kwani kipindi cha nyuma walikuwa wakitegemea wateja kutoka nje ya nchi ambao walikuwa wakija kutalii ndani ya nchi ambao ndio walikuwa wateja wao wakubwa.

“Kabla ya corona kulikuwa na mwitiko mkubwa kwa wateja wetu, kutokana na asilimia sabini, themanini tulikuwa tunategemea ni watalii kutoka njee kwa asilimia thelathini ni wateja wa ndani ya nchi,likini kwa kipindi hiki cha corona biashara imekuwa ni ngumu’’ Gwendo.

Mtandao wa Dodoma New Blog umezungumza na Lukas Sospeter ambaye ni Mfanyabiashara wa Duka la nguo hapa jijini Dodoma anasaluni yake ya kike pia, amesema kwa sasa hali ya biashara imeshuka na hiyo ni kutokana na kuibuka kwa janga hili la corona huku akigusia zaidi kwenye biashara ya saluni za kike namna ambavyo zimeathirika zaidi na tatizo hilo.

Kuna changamoto na hili janga la corona kila mtu anaogopa kiujumla biashara imekuwa haiko sawa kama alivyokuwa zamani hususani kwenye biashara ya saluni za kike’’ Sospeter.

Naye Abel Majiko ambaye ni mfanyabiashashara katika soko kuu la majengo ambaye amekuwa akijihusisha na uuzaji wa majiko katika soko hilo amesema kuwa kutokana na janga hilo la ugonjwa corona hali imekuwa mbaye katika biashara yao lakini bado aendelea kufanya kazi kama kawaidia huku akimshukuru Rais wa Jamhuari ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuwasisitiza watanza kuendelea kufanya kazi kwa bidi licha ya uwepo wa ugonjwa huo.

“Kama nilivyo sema awali hali ni ngumu kwasababu sisi tunategemea wateja kutoka vijijini sasa hivi wanashindwa kuja kwasababu wanasema kuwa mjini kuna corona’’ Majiko.

Ikumbukwe kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh Dkt. John Pombe Magufuli licha ya uwepo wa ugonjwa huo aliwahimiza watanzania kuendelea kufanya kazi kwa bidii ili kuijenga nchi.

“Ugonjwa huu kamwe usiwe kigezo ama sababu ya kuacha kufanya kazi, badala yake utupe hamasa zaidi ya kuchapa kazi, kama mnavyo jionea wenyewe tangu ugonjwa huu uaze kila nchi imekuwa ikichukua tahadhari yake wenyewe’’ Magufuli. 

MWISHO

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.