Na.
Revocatus Kassimba, TANGA
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Gerald Kusaya ameipongeza Menejimenti ya Bodi ya
Mkonge na watumishi kwa kutekeleza agizo la Waziri Mkuu la kuhamia katika ofisi
iliyotwaliwa na serikali hivi karibuni kutoka kwa wamiliki binafsi.
Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe.Martin Shigela (katikati)
akiongoza mazungumzo na Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo kuhusu mkakati wa kuinua
zao la mkonge mkoa wa Tanga
Kusaya
ametoa pongezi hizo jana Jijini Tanga wakati alipokwenda kufanya ufuatiliaji wa
utekelezaji wa maagizo yaliyotolewa na Waziri Mkuu mwezi Machi mwaka huu
kufuatia ripoti ya kamati ya uchunguzi kuhusu mali za bodi ya mkonge
kumilikishwa kwa watu binasfi kinyume cha utaratibu.
“Nawapongeza
menejimenti mpya ya Bodi ya Mkonge kwa kutekeleza kwa vitendo agizo la Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa la kuhamia katika jengo hili na kuendelea na kazi za
kusimamia zao la mkonge”alisema Kusaya.
Waziri
Mkuu aliagiza kuwa jengo lililokuwa linamilikiwa visivyo halali na Willian
Kimweli Madundo na kulitumia kama Medicare hospital Tanga litumike kuwa makao
makuu ya bodi kwani miaka ya nyuma ndipo palikuwa makao makuu ya Mamlaka ya Mkonge
Tanzania.
Aidha,
Katibu Mkuu huyo aliigiza bodi ya mkonge kuhakikisha inafuatilia mali zake
ikiwemo nyumba 32 ambazo zilirejeshwa serikalini “nataka waliokuwa wamiliki
wapewe notisi na kuondoka au wapewe mikataba ya upangaji haraka” alisisitiza.
“Bado
kuna nyumba mbili nchini Uingereza,nataka zirejeshwe serikalini na zile nyumba
mbili jirani na Mkonge hotel hapa Tanga zifuatiliwe kujua uhalali wa umiliki
wake “ alisema Katibu Mkuu huyo.
Kwa
upande wake Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Mkonge Saad Kambona alimweleza
Katibu Mkuu kuwa tayari wameanza kufanya kazi kwenye jengo jipya la ofisi kama
walivyoagizwa na wamefanya ukarabati mdogo kuwezesha jengo hilo kutumika kama
ofisi badala ya ofisi za zamani uwanja wa gofu Tanga.
Kambona
alisema kwa sasa wanaiomba serikali kuendelea kuiwezesha bodi ili iweze kuhudumia
zao la mkonge wakati ikijipanga kuanza kujitegemea kimapato.
"Tuna
lengo baada ya kuimarisha usimamizi wa zao la mkonge nchini,bodi iweze kutoa
gawio kwa serikali “alisema Kambona.
Katika
hatua nyingine Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martin Shigela aliipongeza Wizara ya
Kilimo kwa jitihada zake za kufufua zao la mkonge kwani ndio uti wa mgongo
wawananchi wa Tanga.
Shigela
alisema ni wakati sasa wizara ya kilimo ikaongeza msukumo katika kuhakikisha
mbegu za mkonge zinapatikana kwa wingi na wakulima wanazipata kwa gharama
nafuu.
Mwisho
Comments
Post a Comment