Wazazi wenye watoto wa ugonjwa wa selimundu washauriwa kuwahudumia vyema watoto wao




Na Jackline Kuwanda, Dodoma

Wazazi wenye watoto ambao wanaugonjwa wa Selimundu (sickle cell) wameombwa kutokukata tamaa katika kuwahudumia watoto hao kwani baadhi ya wazazi hukata tamaa kwa kuhofia kuwa ugonjwa huo ni wa kudumu hivyo hushindwa kuwahudumia watoto vile ambavyo inavyotakiwa.

Kauli hiyo imetolewa na Mwanzilishi wa Taasisi ya sickle Strong Children Zuhura Hasan Makuka wakati akizungumza na Mtandao wa Dodoma News Blog ,ambapo amesema kuwa wengi huusisha ugonjwa huo pia na imani za kishirikina na wakati mwingine husababisha mtafaruko katika familia baaina ya wanafamilia.

Aidha,amesema lengo kubwa la Taasisi hiyo ni kutoa elimu kwa wazazi jinsi ya kuwalea watoto hao namna ambavyo inavyotakiwa ili waweze kuepukana na changamoto ambazo zimekuwa zikijitokeza huku akileza namna ambavyo wanawasaidia watoto wanaoumwa ugonjwa huo na wako katika hali Duni.

Makuka amesema wameendelea kutoa elimu kwa vijana ambao bado hawana wenza kuhakikisha kuwa wanapata wenza ambao hawana vinasaba vya selimundu, ili ikifikia wakati wa kupata mtoto, mtoto anazaliwa akiwa hana ugonjwa huo.

Mbali hilo Zuhura ameiyasa jamii kutokuwa na unyanyapaa kwa watoto wenye maradhi hayo kwani humuathiri mtoto anayeugua kuwa dhaifu zaidi kutokana na maneno anayoyapata kwa jamii iliyomzunguka.

Pia, amesema wamekuwa wakitoa elimu zaidi juu ya kukabiliana na unyanyapa wa mitaani ambao umekuwa ukijitokeza na endapo akikutana na mtu ambaye anamnyanyapa basi ni vizuri akamsimaisha na kumpatia elimu zaidi kuhusiana na hali hiyo.

Hatahivyo,SELIMUNDU ni ugonjwa wa kurithi ambao hutokea baada ya mwili wa binadamu kuwa na upungufu katika umbile la seli, ambapo hubadilika na kuwa nusu duara .

Hali hii ya umbile la seli kufanana na mundu, ndio iliyosababisha iitwe iitwe selimundu au kwa jina la kitaalamu sickle cell.

Ni ugonjwa unaorithishana vizazi kwa vizazi, lakini endapo mzazi mmoja tu akiwa na vinasaba vya ugonjwa huu basi huwa ni vigumu kusababisha mtoto kuvipata, bali endapo wazazi wote wawili ikitokea wana vinasaba hivyo.

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.