Wafanyabiashara Soko la Samaki Feri Wasisitizwa Kunawa Mikono mara kwa mara Kuepuka Virusi vya Corona


Na. Musa Khalid, Dar es salaam.
Maafisa Afya wa Soko la Kimataifa la Samaki Feri Manispaa ya Ilala jijini Dar es salaam wameendelea kusisitiza wafanyabishara wa sokoni hapo kunawa mikono mara kwa mara Ili kuepukana na maambukizi ya kuenea kwa Virusi vya Corona.
Wakizungumza na Mtandao wa Dodoma News jijini Dar es salaam Maafisa Afya hao wamesema wameamua kuwahamasisha wananchi kufata taratibu na sheria zilizotolewa na serikali katika kujikinga na maradhi hayo ya Korona.
Afisa Afya wa soko la  samaki Feri, Harold Samweli amesema kufuatia kutangazwa kwa taarifa ya uwepo wa virusi hivyo nchini walianza kuchukua tahadhari ya kutekeleza maelekezo ya serikali.

Marry Jonathan ni Afisa afya mazingira amesema tahadhari nyingine waliochukua ni kuweka matangazo katika soko zima ili kila mfanyabiashara pamoja na wateja wanapoingia waweze kulisoma na kujikumbusha.

Naye Mkuu wa Soko la hilo la Kimataifa la Samaki Feri, Denis Mrema amesema licha ya kuwapa elimu ya kunawa mikono mara kwa mara pia wanawaelimisha kutokusogelea pasipokuwa na sababu.

Ikumbukwe mpaka sasa Virusi vya Corona vimethibitika na kusababisha vifo kwa baadhi ya mataifa mbalimbali duniani ambapo kwa hapa nchini kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa wataalamu wa afya zaidi ya wagonjwa 14 wamethibitika kuwa na virusi hivyo hivyo tumetakiwa kuendelea kuchukua tahadhari.

MWISHO

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.