Shule Zashauriwa Kutumia Vifaa vya Kisasa katika Ufundishaji


Na. Amiri Kilagalila, NJOMBE

Mbunge wa viti maalum Mkoa wa Njombe (CCM), Neema Mgaya  amesema ili elimu iendelee kukua hapa nchini ni lazima shule mbalimbali zianze kutumia vifaa vya kisasa katika kufundishia kama mbinu mbadala ili wanafunzi waweze kufanya vizuri katika masomo yao kulingana na teknolojia inavyokua kwa kasi duniani.

Amezungumza hayo alipokuwa katika ziara ya kutembelea shule ya sekondari Maria Nyerere ambayo ina mradi wa madarasa matatu yanayogharimu milioni 60, pamoja na shule ya sekondari Wanging'ombe na Ludewa sekondari ambapo amegawa jumla ya tarakilishi (kompyuta)10, vichapishi (Printer) 2, huku akiahidi kufunga mfumo wa interneti katika shule hizo.

Baadhi ya wakuu wa shule  zilizonufaika na misaada hiyo akiwemo mwalimu Optatus Mng'ong'o mkuu wa shule ya sekondari Wanging'ombe pamoja na Paulo Mtunduru mkuu wa shule ya sekondari Ludewa,wanasema kuwa misada hiyo itasaidia kuongeza ujuzi kwa walimu kwani watakuwa na fursa kubwa ya kujisomea kupitia mitandao baada ya uwepo wa computer katika shule zao.


Afisa elimu Wilaya ya Ludewa, mwalimu Matenus Ndumbalo pamoja na afisa elimu sekondari Wilaya ya Wanging'ombe, Joyce Mgonja wameshiriki makabidhiano hayo ambapo wamesema kuwa kulingana na teknolojia inavyokua kwa kasi hivi sasa ni lazima matumizi ya Kompyuta yaongezeke mashuleni ili kutanua uelewa kwa wanafunzi pamoja na walimu na hivyo kusidia kukuza kiwango cha elimu hapa nchini.

MWISHO

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.