Mariam Masenga ''Wengine Wanasema Corona Haiwapati Watu Weusi Hivyo Wanakataa Kunawa Mpaka Walazimishwe na Uongozi tu ''
Na. Mwandishi wetu, DODOMA
PAMOJA na kutolewa kwa elimu mbalimbali na viongozi wa serikali
juu ya kujikinga na virusi vinavyosababisha ugonjwa hatari duniani wa CORONA
bado jamii imekuwa na fikra hasi kwa madai kuwa watu weusi hawawezi kukumbwa na
ugonjwa huo.
Hali hiyo imebainishwa na Mariam Masenga ambaye ni
mmoja wa wasimamizi wa kuwataka wateja na wafanyabiashara kunawa mikono kwa
maji na sabuni katika soko la Bonanza lililopo Jijini Dodoma maarufu kwa
kuuza Samaki, Mbogamboga na Matunda .
Akizungumza na waandishi wa habari alisema kuwa anakumbana na
changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na kukutana na baadhi ya watu ambao
wanakuwa wabishi kunawa mikono kwa madai kuwa watu weusi kamwe ugonjwa huo wa Corona hawawezi kupatwa.
“Kunatakiwa elimu kubwa sana kwa jamii mimi nipo
hapa mlangoni ambako uingia wateja na wafanyabiashara wengi kwa ajili ya
kusimamia watu kunawa mikono changamoto iliyopo ni kwamba wapo wengine ambao ni
wabishi wanakataa kunawa wakidai kuwa eti wananawa kwani kuna chakula? wengine
wanasema eti Corona haiwapati watu weusi hivyo wanakataa kunawa mpaka
walazimishwe na uongozi tu.
“Na sijui nani katoa elimu kuwa watu weusi hawawezi kupatwa na
ugonjwa huu wa Corona, serikali na wataalamu wa afya wanatakiwa kutoa elimu ya
kutosha ili kuondosha ukakasi huo ambao unaopotosha ambao unaendelea kuvumishwa
kuwa watu weusi hawawezi kupatwa na Corona” alisema Mariam.
Hata hivyo kutokana na na kuwepo kwa tishio la ugonjwa hatari
unaotokana na maambukizi ya virusi vya CORONA wafanyabiashara na wateja wa Soko
la Bonanza katika jiji la Dodoma wametakiwa kuzingatia utumiaji wa vitakatisha
mikono pindi wanapoingia sokoni kufanya biashara au kununua bidhaa na
yeyote atakayeonekana kukaidi hataruhusiwa kuingia ndani ya soko hilo.
Hayo yamelezwa na Katibu mkuu wa soko hilo, Dickson
Mwesigwa alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari waliotembelea soko hilo
kwa ajili ya kuangalia taratibu za utumiaji wa vitakatisha mikono kwa ajili ya
kujikinga na gonjwa hatari linalosababishwa na virusi vya Corona unafuatwa.
Mwesigwa alisema kuwa kutokana na kuwepo kwa ugonjwa huo ambao
ni tishio kwa dunia uongozi wa soko umelazimika kuweka vifaa mbalimbali ikiwa
ni pamoja na vitakatisha mikono katika milango miwili ya soko na kuwaweka
wasimamizi ambao wahatahakikisha kila anayeingia sokoni hapo ananawa mikono kwa
kuzingatia maelekezo ya serikali na wataalamu wa afya kwa ujumla.
Alisema kuwa vifaa hivyo ambavyo vimwekwa katika milango maalumu
ya kuingilia katika soko hilo na kuwaweka wasimamizi ni wajibu wa kila mmoja
kuhakikisha ananawa mikono pindi anapotaka kuingia ndani ya soko na bila kujali
anayeingia sokoni ni mfanya biashara au ni mteja.
“Sokoni tunapokea watu wengi, huwezi kujua nani mwathirika na ni
nani ambaye yupo salama kutokana na hali hiyo uongozi wa soko la bonanza ambalo
ni maarufu kwa kuuza samaki, matunda na mbogamboga ,tumeamua kutekeleza kwa
vitendo maagizo ya serikali na wataalamu wa afya kwa kuweka vifaa mbalimbali
vya kujikinga na ugonjwa huo.
“Katika soko kuna milango miwili ya kuingilia na kila mlango
tumeweka vitakatisha mikono na tumeweka watu wa kusimamia haijalishi wewew ni
mfanyabiashara au ni mteja nilazima kunawa mikono kwa sababuni na maji tililika
kwa afya ya mtu mwenyewe na kwa usalama wa watu wote waliopo sokoni” alisema
Katibu Mwesigwa.
Hakizungumzia hali ya biashara Mwesigwa alisema kuwa baada ya
kutokea ugonjwa huo biashara ilionekana kuzorota kutokana na jamii jujawa hofu
na kudhani kuwa maambukizi ya Corona yanatokana na hewa.
“Kabla ya serikali kufunga shule, vyuo vya elimu ya juu na kati
pamoja na kutangaza aina ya mikusanyiko isiyotakiwa hali ilikuwa mbaya sana
sokoni watu walikuwa hawaji kununua bidhaa, lakini baada ya serikali kutangaza
kufunga vyuo , shule za msingi na kutangaza aina ya mikusanyiko na kuyaacha
masoko bila kuyafunga angalau sasa wateja wameweza kuja sokoni angalau biashara
imeanza kuwa nzuri japo siyo sana na mzunguko wa hela kwa sasa ni
mdogo” alieleza Mwesigwa.
MWISHO
Comments
Post a Comment