JAMII YAASWA KUTOFUMBIA MACHO VITENDO VYA UKATILI WA KIJINSIA


Na. Jackline Kuwanda, DODOMA

Jamii imeshauriwa kutofumbia macho vitendo vya ukatili wa kijinsia ambavyo vimekuwa vikijitokeza katika maeneo yao badala yake watoe taarifa sehemu husika ili hatua stahiki zichukuliwe.

Ushauri huo umetolewa na Lazaro Leonarld ambaye ni  mwanaharakati anayehusika na masuala ya kutoa elimu kuhusiana na vitendo  vya unyanyasaji na ukatili wa kijinsia wakati akizingumza na Mtandao wa Dodoma News Blog.


Aidha, amesema  kuwa watu wengi hushindwa kusema ukweli kutokana na vitendo hivyo wakihofia ya kuwa jamii itawachukulia tofauti na kwa hali hiyo itakuwa ni ngumu kutokomeza vitendo hivyo.

Wakati huo huo amesema kuwa wanaongoza kufanyiwa vitendo hivyo mara nyingi wamekuwa ni watoto wa kiume na wakike lakini wakiume wamekuwa wakifanyiwa ukatili wa kijinsia mara nyingi na wengi wao wamekuwa wakipata madhara makubwa na ameendelea kuiasa jamii kutofumbia macho vitendo hivyo.

Katika hatua nyingine amesema vyombo ambavyo vinamamlaka ya kusimamia masuala hayo ya ukatili wa kijinsia viendelea kusimamia kikamilifu na wale ambao watabainika kuwa wamekuwa na hatia ya kutenda makosa hayo hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao.


Hatahivyo,amesema ameendelea kutoa elimu katika shule mbalimbali na mwamko wa upokeaji wa elimu wa masuala ya unyanyasaji na ukatili wa kijinsia ni mkubwa.

MWISHO

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.