BUNGE KUSHAURINA NAMNA YA KUWAPIMA WABUNGE MAAMBUKIZI YA COVID -19




Na Mwandishi wetu,Dodoma


SPIKA wa Bunge JOB NDUGAI amesema bunge linatarajia kushauriana na serikali kuangalia namna ya kuwapima wabunge wote endapo wana maambukizi ya Virusi vya Ugonjwa wa Corona(COVID 19).


Uamuzi huo unafuatia baada ya ushauri uliotolewa na mbunge wa jimbo la Kawe HALIMA MDEE aliyeshauri wabunge kupimwa na kuiomba serikali kutoa taarifa ya hali ya maambukizi ya virusi hivyo ilivyo nchini kwa sasa.


Akitolea jibu ushauri huo leo bungeni  jijini Dodoma NDUGAI amesema pamoja na kwamba huwenda maabara ya Taifa itakuwa na foleni ya vipimo vingi lakini watashauriana na wizara husika ili kuona namna bora ya kulitekeleza hilo na kuwataka wabunge kuwa wamoja katikak ipindi hiki.


Amewataka wabunge kuchukua tahadhari ya kukaa umbali wa mita moja baina ya mtu na mtu ili kuchukua tahadhari ya virusi ikiwa ni namna ya kufuata maelekezo yanayotolewa na wataalam wa afya.


Pamoja na hilo amewataka wabunge kuendelea kutoa elimu kwa wananchi wao juu ya namna bora ya kujiepusha na msongamano ili wajikinge dhidi ya maambukizi ya virusi hivyo.

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.