Wahasibu, Wakaguzi wa TAA tumieni vyema mafunzo ya IPSAS - Kaimu Mkurugenzi Mkuu


Na. Bahati Mollel, TAA
WAHASIBU na Wakaguzi wa Ndani wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), wametakiwa kutumia vyema mafunzo ya uandaaji na uwakilishwaji wa vitabu vya Hesabu za fedha kwa kuzingatia viwango vya Kimataifa vya Uhasibu kwa Taasisi za serikali (IPSAS accrual) katika kuboresha ufanisi wao wa kazi wa kila siku, yaliyofungwa leo kwenye Jengo la Pili la Abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA-TB2).
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Mhandisi Mbila Mdemu leo akizungumza na Wahasibu na Wakaguzi wa Ndani waliokuwa wakishiriki mafunzo ya uandaaji na uwakilishwaji wa vitabu vya Hesabu za fedha kwa kuzingatia viwango vya Kimataifa vya Uhasibu kwa Taasisi za serikali (IPSAS accrual), wakati akiyafunga kwenye Jengo la Pili la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA-TB3)
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TAA, ambaye pia ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Uhandisi na Huduma za Ufundi, Mhandisi Mbila Mdemu alisema amesema kuwa mafunzo hayo yawe chachu ya kuwabadilisha na kupunguza hoja za ukaguzi.

“Ninaimani nyote hapa mlishiriki kuanzia siku ya kwanza ya mafunzo haya ya siku tano hadi mwisho mukiwa na afya njema, hivyo tujitahidi kama wahasibu tusizalishe hoja za kizembe na tuhakikishe tunasimama kwa miguu yetu kwa kufanya kazi kwa kiwango na uharaka,” alisisitiza Mhandisi Mdemu.

Amesema mafunzo haya yamekuja wakati muafaka, ambapo pia yameweza kushirikisha washiriki kutoka viwanja vyote vilipocho chini ya TAA, ambapo awali kulikuwa na changamoto chache katika hesabu na kusababisha kuwe na dosari wakati wa ukaguzi.
Wahasibu na Wakaguzi wa Ndani wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), wakimsikiliza Mkufunzi CPA Angelile Tende (hayupo pichani) katika mafunzo ya uandaaji na uwakilishwaji wa vitabu vya Hesabu za fedha kwa kuzingatia viwango vya Kimataifa vya Uhasibu kwa Taasisi za serikali (IPSAS accrual). Mafunzo hayo yamemalizika leo kwenye Jengo la Pili la Abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA_TB2)
“Mafunzo yatakuwa yamewaongezea ujuzi wa hali ya juu na mtaweza kusaidiana wenyewe kwa wenyewe maana mmeshiriki wahasibu wa viwanja vyetu vyote pia wakaguzi wetu wa ndani nao wameshiriki, hivyo kwa njia moja ama nyingine tutakuwa katika nafasi nzuri ya kupunguza ama kuondoa kabisa hoja za ukaguzi,” amesema.

Pia aliwashukuru wakufunzi kutoka Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi Tanzania (NBAA), kwa kuendesha mafunzo hayo.

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Fedha na Biashara, CPA Josephine Kolola aliishukuru Mamlaka kwa kukubali kufanyika kwa mafunzo hayo muhimu na ameahidi kuwa watazingatia na kufanyia kazi vyote walivyo fundishwa.
Mkufunzi CPA Angelile Tende kutoka Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi Tanzania (NBAA), akiwafundisha Wahasibu na Wakaguzi wa Ndani wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), wakimsikiliza Mkufunzi CPA Mohamed Nusura (hayupo pichani) mafunzo yaliyomalizika leo ya uandaaji na uwakilishwaji wa vitabu vya Hesabu za fedha kwa kuzingatia viwango vya Kimataifa vya Uhasibu kwa Taasisi za serikali (IPSAS accrual), kwenye Jengo la Pili la Abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA_TB2)
“Tunaomba utufikishie salamu zetu kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka na tunaahidi matunda ya mafunzo haya atayaona kwa Wahasibu wameiva na anaamini hoja za ukaguzi zitapungua na hata kuondoka kabisa,” amesema CPA Kolola.

MWISHO      

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.