SHIRIKA LA SUMA JKT LAJIENDESHA KWA FAIDA NCHINI


Na. Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Brigedia Jenerali Charles Mbuge amesema uwepo wa walinzi SUMA GARD zaidi ya elfu kumi nchi nzima kumesaidia shirika la SUMA JKT kujiendesha katika shughuli zake za kiulinzi na hatimaye kupata faida kubwa.

Lengo la kuanzishwa kwa SUMA JKT ni kusaidia miradi ambayo ina uwezo mkubwa wa uzalishaji ili iweze kuzalisha zaidi na kwa faida na hivyo kuisaidia Serikali katika kupunguza matumizi ya kuendesha shughuli za JKT, alisema.

Brigedia Generali Mbuge ametoa kauli hiyo Jijini Dar Es Salaam katika uzinduzi wa magari manne na pikipiki tano zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni mia sita ili kutekeleza kwa vitendo, nia ya Serikali  ya kukuza uchumi wa nchi katika Viwanda na Biashara  kwa maendeleo ya nchi.

Brigedia Jenerali Mbuge amezitaka taasisi mbali mbali za serikali na binafsi kuwatumia walinzi wa SUMA GARD ili kupunguza tatizo la ajira kwa vijana.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa bodi ya SUMA JKT, Meja Generali mstaafu, Farrah Mohamed amesema Jeshi hilo lina umuhimu mkubwa katika kujenga malezi kwa vijana hapa nchini, hatua ambayo itasaidia taifa kupiga hatua katika maendeleo kwa haraka zaidi.

MWISHO

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.