"WANAFUNZI WA KIKE MSIJIRAHISISHE TUPUNGUZE UKATILI" DC KASESELA


Na. Mwandishi Wetu, IRINGA
Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Mhe. Richard Kasesela amewataka wanafunzi wa kike kutojirahisisha mpaka kupelekea kufanyiwa vitendo vya ukatili dhidi yao.
Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mhe. Richard Kasesela akizungumza na wanafunzi
wa shule za Sekondari za Wilaya ya Iringa katika Kongamano la wanafunzi la
kuupokea msafara wa kijinsia mkoani hapo
Ameyasema hayo leo mkoani Iringa wakati akiupokea msafara wa kijinsia wa kutokomeza ukatili wa kijinsia uliposimama mkoani hapo.
Ameongeza kuwa vitendo vya kikatili vimekuwa vikiongezeka siku hadi siku hasa katika familia na vimekuwa vikifumbiwa macho na kumalizana kimya kimya.
"Msijirahisishe watoto wangu mnatupa tabu sana maana tumekuwa tunapambana na vitendo vya ukatili ninyi mnajirahisisha" alisema.
Mhe. Kasesela amesema kuwa kumekuwa na ongezeko la mimba na ndoa za utotoni na ulawiti kwa watoto wa kiume watoto wamekuwa wameharibiwa na kusbabishiwa maumivu na ukatili wa kisaikolojia.
Baadhi ya wanafunzi wa shule za Sekondari Wilaya ya Iringa wakifuatilia ujumbe
wa Msfara wa kijinsia kutokomeza ukatili katika Kongamano la wanafunzi
Ameongeza kuwa Serikali imejipanga katika kuhakikisha inasimamia ustawi wa jamii ikiwemo kuwalinda na vitendo vya kikatili dhidi yao hasa kwa makundi maalum ya wanawake, Watoto na walemavu.
"Tusikae kimya tuseme tutoe taarifa kwa vyombo vya kisheria kuhusu vitendo vya kikatili vinavyotokea katika familia na jamii zetu" alisema.
Naye Mwakilishi wa Katibu Mkuu Idara Kuu Maendeleo ya Jamii Bi. Imelda Kamugisha amesema vitemdonvyabukatili.vimekuwa vikitokea kwenye jamii zeru na kwa mujibu wa takwimu wanawake asilimia 30 walio kwenye ndoa wanafanyiwa ukatili wa kijinsia.
"Kutokana na kuongezeka kwa vitendo vya ukatili Serikali imeongeza vituo vya huduma jumuishi na namba ya kutoa ripoti ya vitendo vya ukatili kwa watoto ili kuweza kuchukua hatua katika mapambano dhidi ya vitendo vya kikatili" alisema.
Kwa upande wake Wakili kutoka Wakala wa Usajili, Ufilisi na udhamini RITA, Janeth Mandawa ametoa wito kwa wanaume kuandika wosia ili kuondokana na vitendo vya kikatili vinavyowakumba wanawake wajane katika jamii zetu ili kuwezesha kuwapa haki zao stahili.
Msanii Nurdin Bilal "Shetta" akitumbuiza katika Kongamano la wanafunzi
Wilayani Iringa la kuupokea msafara wa kijinsia mkoani hapo
"Sisi tunahusika na masuala ya wosia kuandika wosia sio kufa ila inasaidia kutoa maelekezo baada ya mume au mke kufariki ili tuondokane na vitendo vya ukatili"alisema.
 MWISHO


Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.