KWARESMA FURSA TUJITAFAKARI NA KUMPA MUNGU NAFASI YA KWANZA


Na. Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC) Padre Dkt. Charles Kitima amesema kipindi cha kwaresima ni fursa ya kujitafakari na kumpa Mungu nafasi ya kwanza katika maisha ikiwa ni pamoja na kutambua nafasi ya mwenyezi katika maisha ya kila siku kwa wakristo na wasio wakristo.

Padre Dkt. Kitima ametoa kauli hiyo wakati wakristo wakielekea katika mwezi wa toba ambapo amewataka waumini kote nchini kutambua nafasi ya muumba katika maisha yao pamoja na kubadilisha mahusiano yao mabaya na Mwenyezi Mungu.

Kwa upande wake, Padre Hesco Msaga amesema kipindi cha kwaresma ni safari ya kiroho ambayo kila mkatoliki anatakiwa kutafakari na kujiandaa nafsi yake na kujiweka tayari katika kipindi hiki cha toba.

Baadhi ya wakristo wameelezea namna wanavyoutambua umuhimu wa kwaresima.

MWISHO

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.