BIMA INA UMUHIMU KATIKA KUJENGA UCHUMI


Na. Jackline Kuwanda, DODOMA   

Bima ni sekta ndogo ya fedha yenye umuhimu mkubwa katika Kujenga uchumi na kuchangia pato la Taifa nchini.

Kauli hiyo imetolewa na Meneja wa Mamlaka ya usimamizi wa Bima kanda ya kati (TIRA), Stella Rutahuza wakati akitoa mafunzo ya uelewa wa Bima kwa waandishi wa Habari jijini Dodoma.
Rutahuza amesema kuwa Bima husaidia kupunguza makali ya hasara yanayotokana na majanga. Bima pia husaidia kukuza uchumi na ajira ya kudumu katika Taifa, aliongeza.

Aidha, amesema kuwa Bima zimegawanyika katika makundi mawili. Alitayaja makundi hayo kuwa ni Bima za mali na ajali, ambapo kundi hilo ni la muda mfupi na kwa kawaida bima zake humaliza muda wake katika kipindi kisichozidi miezi 12 haijaendelezwa tena na wahusika katika mkataba.

Wakati huohuo amesema kuwa Bima za mali na ajali ni kama Bima za  vyombo vya moto, meli na mizigo, Ndege, moto. Bima za maisha amezitaja kuwa ni Bima ya maisha na uwekezaji, maisha na vikundi na Bima ya vikundi kwa dhamana ya mkopo.

Akizungumzia Bima ya usafirishaji Rutahuza amesema, Bima hiyo hujumuisha vyombo vya usafiri nchi kavu, reli, ndege, meli, bidhaa zinazo, dhima ya gari, dhima ya ndege na dhima kwa meli.

Akizungumzia misingi ya Bima na namna ya kudhibiti majanga Mkurugenzi wa kuendeleza soko la Bima  na utafiti wa Mamlaka ya usimamizi wa Bima Tanzania, Adelaide Muganyizi amesema ilii mkataba wa Bima ufanye kazi ni lazima uwepo uhusiano unaotambulika kisheria kati ya bima na kinachowekewa Bima.

Lengo la mafunzo hayo kwa wanahabari ni kuwajengea uwezo na uelewa ili kuweza kufahamu masuala ya Bima na wao kutoa elimu kwa jamii ili jamii iweze kutambua faida ya kuwa na Bima katika Maisha yao ya kila siku.

MWISHO

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.