BERNARD MEMBE AVULIWA UANACHAMA CCM


Na. Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) imemvua uanachama Waziri wa zamani wa Mambo ya Nje, Bernard Membe.
Bernard Membe
Hayo yameelezwa leo na katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika katika ofisi ndogo za CCM zilizopo mtaa wa Lumumba  hapa jijini Dar es Salaam.
Polepole ameeleza uamuzi wa kamati kuu ambayo ilitoa siku saba kwa kamati ya nidhamu iliyowahoji vigogo hao kukamilisha suala lao na kuwasilisha taarifa.
Wakati Membe akivuliwa uanachama, katibu mkuu wa zamani wa CCM, Abdulrahman Kinana amepewa karipio na kutakiwa kutogombea nafasi yoyote ndani ya chama hicho kwa miezi 18 huku katibu mkuu mwingine wa zamani Yusufu Makamba akisamehewa.
Vigogo hao walihojiwa baada ya sauti zao kusambaa katika mitandao ya kijamii wakieleza jinsi CCM inavyopoteza mvuto na jinsi chama kilivyoshindwa kuwalinda makatibu hao dhidi ya mtu anayejiita mwanaharakati, ambaye alikuwa akitoa tuhuma dhidi yao.
MWISHO

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.