YALIYOJIRI WAKATI WA KIPINDI CHA TUNATEKELEZA KILICHOMSHIRIKISHA MKUU WA MKOA WA NJOMBE, CHRISTOPHER OLE SENDEKA JANUARI 30, 2020



# Bilioni zaidi ya 500 zimetolewa na Serikali katika ujenzi wa miundombinu ya barabara kwa kiwango cha lami kuunganisha Wilaya zote na makao makuu ya mkoa

#Serikali ya Awamu ya Tano imetimiza matarajio ya wananchi wa mkoa wa Njombe kupitia ujenzi wa miundombinu ya barabara, vituo vya afya, maji na elimu 

#Mkoa wa Njombe uko salama hali inayowezesha wananchi kutekeleza shughuli za uzalishaji na kujiletea maendeleo 

#Ujenzi wa miundombinu ya barabara unawezesha utekelezaji wa miradi ya kimkakati kama ule wa Chuma cha Liganga na Mchuchuma kwa maslahi ya Taifa 

#Jengo la wagonjwa wa nje (OPD)limekamilka na kuanza kutoa huduma kwa wananchi 

#Bilioni 4.5 zilitolewa na Serikali kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali za Wilaya 

#Vituo 7 vya afya vimepatiwa fedha za upanuzi katika mkoa wa Njombe 

# Mkoa wa Njombe umefanikiwa katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo 

# Ujenzi wa miundombinu utawezesha kukua kwa biashara katika mkoa wa Njombe 

# Tumejenga kiwanda kipya cha kusindika chai katika mkoa wetu na pia tumejenga viwanda vya kati na vidogo 

#Tumepata kiwanda cha kuzalisha mafuta yanayotokana na zao la parachichi 

# Kiwanda cha kufungasha maparachichi na kusafisha nje ya nchi nacho kinafanya kazi vizuri 

# Mwitikio wa wananchi kuzalisha zao la parachichi ni mzuri na mkoa umeweka utaratibu wa kuwafuatilia na kuwasaidia 

# Mkoa wa Njombe unanufaika na mradi wa gridi ya Taifa kutoka kituo cha kupoza umeme Makambako hivyo kuna umeme wakutosha 

# Mkoa wa Njombe una maeneo mazuri ya uwekezaji, hivyo tunawakaribisha wawekezaji wa ndani na nje 

Imeandaliwa na Idara ya Habari MAELEZO

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.