Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na
Mazingira), Mussa Azzan Zungu amemtaka kila mtumishi katika Ofisi hiyo
kuwajibika ipasavyo mahali pa kazi na kuepuka kujihusisha na vitendo
visivyokuwa vya kimaadili.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mussa Azzan Zungu akifungua mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi hiyo |
“Ninafahamu kwamba watumishi wana malalamiko
yanayohusu kutopandishwa vyeo kwa muda mrefu na upungufu wa watumishi katika
Idara na Vitengo, malalamiko haya ni mtambuka katika Wizara zote kwani
yametokana na uhakiki wa vyeti vya elimu ya sekondari na ualimu zoezi
lililoendeshwa na Serikali kuanzia mwaka 2016. Ninawasihi muwe na subira wakati
Serikali ikiimarisha mifumo yake ya Usimamizi wa Rasilimaliwatu,” alisisitiza.
Aidha, Waziri Zungu alibainisha kuwa Baraza la
wafanyakazi ni jukwaa muhimu mahali pa kazi kwani ni kiunganishi kati ya
Menejimenti na Wafanyakazi hivyo aliwataka kuendeleza ushirikiano ili kuleta
ufanisi katika kutekeleza majukumu ya Ofisi na Taifakwa ujumla.
“Watumishi wenzangu hakikisheni mshahara mnaopewa
mnautendea haki! Msitake kupata mshahara wa bure! Fanyeni kazi kwa bidii” Zungu
alisisitiza.
Aliongeza kuwa kuwepo kwa Mabaraza ya Wafanyakazi
katika Taasisi ni takwa la Kisheria kwa madhumuni ya kuishauri Serikali katika
ngazi za Idara na Ofisi ambapo malengo yake ni kuhakikisha kuwa majukumu yanatekelezwa
ipasavyo, kulinda haki na wajibu wa waajiri na wafanyakazi, kutoa ushauri
kuhusu kujenga mazingira bora ya kazi, maslahi ya watumishi na kusimamia haki
na ustawi katika sehemu za kazi.
Aliwakumbusha kuwa wajibu wa Mabaraza haya kama
vyombo vya ushauri na usimamizi ni kuhakikisha kuwa waajiri na watumishi
wanatambua wajibu na haki zao na kuzingatia maadili ya utumishi wao ili kuleta
matokeo chanya katika utendaji kazi.
![]() |
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mussa Azzan Zungu akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi hiyo baada ya kufungua mkutano |
MWISHO
Comments
Post a Comment