WAZIRI MKUU AAHIDI KULINDA WAWEKEZAJI WA NDANI NCHINI


Na. Mwandishi Wetu, DODOMA 
WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amesema kama msimamizi wa utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ataendelea kulinda wawekezaji wa ndani na atakuwa mkali pale anapoona kuna mambo hayaendi sawa.

Majaliwa ametoa msimamo huo leo bungeni mjini Dodoma wakati akijibu swali la papo kwa papo la Mbunge Jaku Ayoub aliyetaka kufahamu ni lini Serikali itafikiria Sukari inayozalishwa katika kiwanda cha Mahonda Zanzibar angalau kidogo ikaja kuuzwa Tanzania Bara kama ilivyo kwa bidhaa nyingine zinazozalishwa Tanzania Bara kuuzwa Zanzibar.

Akijibu swali hilo Waziri Mkuu amesema alipofanya ziara alikuta sukari nyingi ipo bohari imejaa na kwamba kiwanda hicho kina uwezo wa kuzalisha tani elfu 24,000 lakini hivi sasa kinazalisha tani 6,000.

MWISHO

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.