Veronica Simba, DODOMA
🔷
*Wenye utendaji duni wawajibishwe*
🔷
*Wakamilishe kazi Aprili, 2020*
🔷
*Wananchi visiwani watozwe bei ya umeme iliyopitishwa na serikali*
Waziri wa Nishati Dkt Medard Kalemani akizungumza na wakandarasi wanaotekeleza miradi ya umeme vijijini, awamu ya tatu, mzunguko wa kwanza (REA III-Round 1), jijini Dodoma |
Waziri wa Nishati Dkt Medard Kalemani
amekutana na wakandarasi wanaotekeleza miradi ya umeme vijijini awamu ya tatu
mzunguko wa kwanza na kuwapa maagizo mazito yanayolenga kuhakikisha mradi
unakamilika kwa wakati na viwango stahiki.
Mkutano huo uliofanyika jijini Dodoma, umehudhuriwa pia na Naibu Waziri wa Nishati, Subira
Mgalu, Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara husika, Mhandisi Leonard Masanja, Bodi za
Wakurugenzi na Menejimenti za Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Shirika la
Umeme Tanzania (TANESCO) pamoja na wasimamizi wa miradi husika kutoka wizarani,
TANESCO na REA.
Moja ya maagizo aliyoyatoa Waziri ni
kwa watendaji wakuu wa TANESCO na REA, kuziwajibisha kampuni tatu za
wakandarasi ambazo utendaji kazi wake hadi sasa uko chini ya wastani kwa mujibu
wa mikataba yao waliyosaini.
Amezitaja kampuni hizo kuwa ni Urban & Rural Engineering Ltd ambayo utendaji wake katika wilaya za Kakonko na Kibondo mkoani Kigoma uko chini; JV Pomy Engineering Co. Ltd, Intercity Builders Ltd & Octopus Engineering Ltd (Kaliua, Tabora) pamoja na NIPO Group Ltd (Arusha).
Amezitaja kampuni hizo kuwa ni Urban & Rural Engineering Ltd ambayo utendaji wake katika wilaya za Kakonko na Kibondo mkoani Kigoma uko chini; JV Pomy Engineering Co. Ltd, Intercity Builders Ltd & Octopus Engineering Ltd (Kaliua, Tabora) pamoja na NIPO Group Ltd (Arusha).
Akifafanua, Waziri Kalemani ameeleza
kuwa, kampuni hizo tatu ni miongoni mwa kampuni saba ambazo zilibainika kufanya
kazi chini ya kiwango na serikali ikatoa maelekezo kuwa zifanye marekebisho ya
kuboresha utendaji wao ndani ya siku 14; hata hivyo ni kampuni nne tu kati ya
hizo zilitimiza maelekezo husika.
“Nazidi kuelekeza; siku 14 mlizowapitia
kwa barua zenu, kulingana na mkataba zikikamilika pasipo wao kurekebisha dosari
hizo; chukueni hatua ya kufuta mikataba yao au kusitisha malipo yao pamoja na
kutoa adhabu kulingana na mkataba ulivyo.”
Sambamba na maagizo ya kuziwajibisha
kampuni hizo zenye utendaji duni, Waziri amezipongeza kampuni tano ambazo
zimefanya vizuri kwa kuvuka kiwango cha mkataba hadi kufikia sasa.
Amesema, kwa mujibu wa mkataba, wakandarasi wote wanapaswa kukamilisha kazi ifikapo Juni mwaka huu lakini kampuni hizo zimevuka lengo kwa baadhi yake kukamilisha kazi kwa asilimia 100 hadi sasa, ikiwa ni miezi mitano kabla ya makubaliano na nyingine kufikia kiwango cha juu kabisa zikielekea kukamilisha kazi husika ndani ya muda mfupi ujao.
Amesema, kwa mujibu wa mkataba, wakandarasi wote wanapaswa kukamilisha kazi ifikapo Juni mwaka huu lakini kampuni hizo zimevuka lengo kwa baadhi yake kukamilisha kazi kwa asilimia 100 hadi sasa, ikiwa ni miezi mitano kabla ya makubaliano na nyingine kufikia kiwango cha juu kabisa zikielekea kukamilisha kazi husika ndani ya muda mfupi ujao.
Kampuni hizo ni STEG International
Services waliotekeleza mradi kwa asilimia 100 katika mikoa ya Songwe na Mbeya;
Sengerema Engineering Group Ltd, mkoani Pwani (zaidi ya 99%); Derm Electrics
Ltd, wilayani Handeni (99.2%); JV White City International Contractors and
Guangdong Co. Ltd, wilayani Simiyu (96%) pamoja na State Grid Electrical &
Technical Work Ltd, mkoani Lindi (97%).
Maagizo mengine aliyotoa Waziri ni kwa
kila mkandarasi kuhakikisha anakamilisha kazi katika eneo lake ifikapo Aprili
mwaka huu ili miezi miwili inayosalia (Mei na Juni) itumike kukamilisha
marekebisho madogo madogo kabla ya kukabidhi rasmi ifikapo Juni, 2020.
Sanjari na hilo, amewataka mameneja wa
TANESCO wa wilaya na mikoa pamoja na wahandisi wanaosimamia miradi husika,
kuhakikisha ifikapo Februari 15, mwaka huu pasiwepo na nguzo iliyosimikwa ikiwa
haijafungwa nyaya za umeme, pasiwepo na eneo la mradi lisilo na transfoma na
pasiwepo na eneo la mradi ambalo wateja hawajaunganishiwa umeme.
Aidha, Waziri ameagiza kila mkandarasi kukabidhi Mpango-Kazi wake kwa uongozi wa TANESCO na REA pamoja na Wakuu wa Wilaya ambao unaainisha majina ya vijiji vitakavyounganishiwa umeme kila wiki, kuanzia sasa hadi mwezi Aprili, ambao ndiyo muda wa mwisho kwa kila mmoja kuwa amekamilisha kazi.
Aidha, Waziri ameagiza kila mkandarasi kukabidhi Mpango-Kazi wake kwa uongozi wa TANESCO na REA pamoja na Wakuu wa Wilaya ambao unaainisha majina ya vijiji vitakavyounganishiwa umeme kila wiki, kuanzia sasa hadi mwezi Aprili, ambao ndiyo muda wa mwisho kwa kila mmoja kuwa amekamilisha kazi.
“Taarifa hizo ziwafikie Wakuu wa Wilaya
kabla ya Februari 5, mwaka huu. Niwaombe Wakuu wa Wilaya mfuatilie utekelezaji
wa kazi husika kama ambavyo taarifa itakuwa imeainisha. Mkandarasi akishindwa
kutekeleza kama alivyoainisha, chukueni hatua za kumkamata,” amesisitiza.
Katika hatua nyingine, Waziri amekemea
tabia ya baadhi ya wakandarasi kutotekeleza kazi ipasavyo huku wakitoa
kisingizio cha kutokuwa na vifaa. Alisema, wakandarasi wanapaswa kufahamu kuwa
ununuzi wa vifaa ni jukumu lao maana wote wamelipwa na serikali ili kuwawezesha
kutekeleza kazi zao ikiwemo hiyo ya ununuzi wa vifaa.
Vilevile, ametoa onyo kwa wapimaji wa
miradi ya umeme (surveyors), hususan wale wanaokaa na fomu za wateja zaidi ya
10 kwa muda mrefu pasipo kwenda kutekeleza kazi husika, kuacha tabia hiyo mara
moja vinginevyo watawajibishwa.
Waziri ametoa kalipio kwa mameneja wa TANESCO ambao kwa namna moja au nyingine wanaruhusu wananchi, hususan walioko maeneo ya visiwani kutozwa gharama kubwa za umeme na wazalishaji binafsi.
Waziri ametoa kalipio kwa mameneja wa TANESCO ambao kwa namna moja au nyingine wanaruhusu wananchi, hususan walioko maeneo ya visiwani kutozwa gharama kubwa za umeme na wazalishaji binafsi.
“Nimeambiwa baadhi ya visiwa ikiwemo
Ukerewe, wananchi wanatozwa shilingi 2,500 kwa uniti moja ya umeme jambo ambalo
siyo sawa maana bei iliyopitishwa na serikali kwa wananchi wote ambao matumizi
yao hayazidi uniti 75 kwa mwezi ni shilingi 100 tu kwa kila uniti.”
Hata hivyo, Waziri amezipongeza Bodi,
Menejimenti na wafanyakazi wa TANESCO na REA kwa kufanya kazi nzuri hususan
katika uunganishaji umeme katika maeneo mbalimbali nchini jambo ambalo
limeungwa mkono na Naibu Waziri Mgalu wakati akifunga mkutano huo kwa niaba ya
Waziri.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti,
Waziri na Naibu wake wamesema pamoja na uwepo wa changamoto kadhaa katika
utekelezaji wa miradi ya umeme lakini kwa kiasi kikubwa watendaji husika
wamekuwa wakifanya kazi nzuri sana.
“Kimsingi tunawahitaji sana. Tunahitaji
sana ushirikiano wenu na kujitoa kwenu ili kwa pamoja tufanikishe azma ya Rais
wetu Mheshimiwa Dkt John Pombe Magufuli ya nchi kuwa ya uchumi wa viwanda. Hili
linawezekana kwa uwepo wa umeme wa uhakika na wenye gharama nafuu,” amesema
Naibu Waziri.
Aidha, Naibu Waziri ameipongeza Bodi ya
Wakurugenzi ya REA akisema inapaswa kuigwa kutokana na utendaji kazi wake
mahiri. “Bodi hii inatembelea maeneo mbalimbali ya mradi na kukutana na
watendaji wa pande zote zinazohusika ambazo ni serikali, wakandarasi, wauzaji
na wazalishaji wa vifaa ili kujua changamoto zao na kuzitafutia ufumbuzi.
Naye Kaimu Katibu Mkuu, Mhandisi Masanja amewaasa wakandarasi husika kuhakikisha wanaongeza nguvu katika kukamilisha idadi ya wananchi wanaopaswa kuunganishiwa umeme kwa mujibu wa mikataba yao badala ya kuunganisha wananchi wachache na kuhamia kijiji kingine.
Naye Kaimu Katibu Mkuu, Mhandisi Masanja amewaasa wakandarasi husika kuhakikisha wanaongeza nguvu katika kukamilisha idadi ya wananchi wanaopaswa kuunganishiwa umeme kwa mujibu wa mikataba yao badala ya kuunganisha wananchi wachache na kuhamia kijiji kingine.
Kwa upande wao, watendaji wakuu kutoka
TANESCO, REA na wakandarasi husika wameahidi kutekeleza maagizo yote waliyopewa
na Waziri.
Comments
Post a Comment