WAFANYABIASHARA JIJI LA DODOMA WATAKIWA KUFANYA BIASHARA MAENEO RASMI


Na. Dennis Gondwe, DODOMA
WAFANYABIASHARA katika masoko ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma wametakiwa kufanya biashara zao katika maeneo rasmi waliyotengewa ili kutokwamisha shughuli nyingine za kijamii kuendelea.
Afisa Masoko, James Yuna

Kauli hiyo ilitolewa na afisa masoko wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, James Yuna alipokuwa akihojiwa katika kipindi cha Dodoma ‘Live’ kinachorushwa na kituo cha redio cha Dodoma FM.

Yuna alisema kuwa imezuka tabia kwa baadhi ya wafanyabiashara kupanga biashara zao nje ya maeneo waliyopangiwa katika masoko jijini hapo. “Upangaji wa biashara nje ya masoko ni kinyume na utaratibu. Wapo baadhi ya wafanyabiashara wanaopanga bidhaa zao nje ya masoko na wengine barabarani. Utaratibu huu unazuia huduma nyingine kuendelea katika Halmashauri ya Jiji. Barabarani ni sehemu ya kupita magari na waenda kwa miguu” alisema Yuna.

Kufanyia biashara maeneo hayo tunahatarisha maisha ya wafanyabiashara hao pindi ajali inapotokea, aliongeza. Aidha, kuwa kufanya biashara maeneo yasiyo rasmi kunahatarisha usalama wa bidhaa zinazouzwa ikiwa ni pamoja na usafi.

Afisa Masoko huyo aliwataka wafanyabiashara katika masoko ya jiji hilo kufanya biashara kwa kuzingatia taratibu zilizowekwa.

MWISHO

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.