SERIKALI YATAHADHARISHA WANAFUNZI WANAOSOMA CHINA KUSUBIRI HALI IWE SAWA YA VIRUSI VYA CORONA



Na. Mwandishi Wetu, DODOMA
SERIKALI imewasihi wazazi wenye watoto wanaosoma nchini China waliorudi kwa ajili ya likizo kutowaruhusu kurudi mpaka hapo watakapopata mawasiliano ya kidiplomasia kuhusu maendeleo ya mlipuko wa ugonjwa wa homa kali ya mapafu inayosababishwa na kirusi aina ya ‘Corona’.

Tahadhari hiyo ameitoa jana bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la papo kwa papo la Mbunge wa Mafinga Mjini, COSATO Chumi aliyetaka kujua serikali imejipangaje kukabiliana na kudhibiti virusi vya ugonjwa huo ambao kwa namna moja ama nyingine unaathiri ukuaji wa maendeleo wa Taifa na wananchi kwa kukizingatia kuna biashara kubwa kati ya Tanzania na China.

Waziri Mkuu amekiri kuwa ni kweli kwamba China kuna ugonjwa wa virusi ya ‘Corona’ unaopoteza maisha ya watu na sasa wameanza kuona nchi za jirani yake wameanza kupata maambukizi hayo.

Amewahakikishia kuwa Tanzania haina ugonjwa huo wa ‘Corona’ na jana Waziri wa Afya na Naibu Waziri wa Afya wametoa taarifa za ugonjwa huu.

MWISHO

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.