SERIKALI YAONGEZA UMAKINI UTOAJI VITAMBULISHO VYA TAIFA


Na. Mwandishi Wetu, DODOMA 
WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amesema serikali imeongeza umakini katika utoaji wa vitambulisho vya Taifa katika mikoa iliyopo mipakani na hivyo kuwataka watanzania kusaidia kuwatambua watu wasio raia wa Tanzania ambao wanachukua vitambulisho vya uraia ili kudhibiti hali ya ulinzi na usalama ndani ya nchi.

Waziri Mkuu amesema hayo leo bungeni jijini Dodoma katika kipindi cha maswali ya papo kwa papo wakati akijibu swali la mbunge wa Buhigwe, Obama Ntabaliba aliyetaka kujua kauli ya serikali katika kuhakikisha wananchi wanapata vitambulisho vya NIDA.

Amesema upo ukweli kwamba watanzania wengi walikuwa hajawafikiwa kupata vitambulisho vya Nida mpaka ngazi ya vijiji na vitongojini jambo ambalo serikali imelifanyia kazi kwa kuongeza idadi ya watumishi kwenye ngazi za halmashauri ili kuweza kufika kwenye vijiji na vitongoji.

Aidha, amesema serikali imeridhia kutumika kwa namba ya kitambulisho pale palipo na uhitaji kama mwananchi atakuwa hajapata kitambulisho na kusisitiza utekelezaji wa maelekezo waliyotoa ikiwemo kubandikwa orodha ya wananchi na namba zao ili kuweka urahisi wa upatikanaji wa namba hizo kwa wananchi.

MWISHO

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.