OFISI YA UKAGUZI YATAKIWA KUWA MSTARI WA MBELE MAPAMBANO YA UKIMWI


Na. Jackline Kuwanda, DODOMA 

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Mary Maganga amelihimiza baraza la wafanyakazi la Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi kuwa mstari wa mbele katika mapambano dhidi ya rushwa.

Pia amelitaka baraza Hilo kufanya kazi kwa kuzingatia  uwajibikaji na misingi ya  Maadili  kwani ni nguzo muhimu kwa maendeleo ya Taifa.

Akizungumza Jijini Dodoma  wakati  akifungua mkutano  wa kwanza wa baraza la wafanyakazi  wa ofisi ya Taifa ya Ukaguzi 2019/2020,  amesema  ni muhimu kwa baraza hilo kufanya kazi kwa maadili  na nidhamu ya hali ya juu kwani ni jicho la watanzania  katika masuala ya ukaguzi wa rasilimali za umma.
Kwa upande wake Mdhibiti na Mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali (CAG), Charles Kichere ambaye pia ni mwenyekiti wa baraza la wafanyakazi Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi amesema lengo kuu la mkutano huo ni kupitia na kuidhinisha makadilio ya bajeti ya ofisi ya Taifa ya ukaguzi kwa mwaka wa fedha 2020/2021 kama inavyoelekezwa kwenye waraka  Na.1 wa mwaka 1970.
Katika hatua nyingine Kichere amesema kuwa  baadhi ya changamoto zinazoikabili ofisi hiyo  ni pamoja na uhaba wa fedha unaokwamisha majukumu ya ofisi ,mgao wa fedha kutokuja kwa wakati na usiotosheleza mahitaji, mishahara midogo kwa wafanyakazi.
Naye, Jenijely James, Katibu wa kamati za Wanawake  -TUGHE Taifa amesema baraza hilo ni nguzo muhimu kwa maendeleo huku Tumainiel Mshomba ambaye ni  ambaye ni katibu wa baraza la wafanyakazi ofisi ya Taifa ya Ukaguzi akisema muundo wa baraza hilo lina wajumbe 110.
MWISHO

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.