KANGI LUGOLA AFIKA MAKAO MAKUU YA TAKUKURU KUHOJIWA


Na. Mwandishi Wetu, DODOMA
ALIYEKUWA Waziri wa Mambo ya ndani ya Nchi, Kangi Lugola leo amefika Makao Makuu ya Ofisi za Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kuhojiwa.

Kangi amehojiwa takribani saa6 Katika Ofisi jizo zilizopo eneo la Jamhuri jijini Dodoma kuanzia majira moja na dakika24 asubuhi kwa ajili ya kuhojiwa ambapo alitoka saa6na dakika35.

Kangi ambaye kwa sasa ni Mbunge wa Mwibara (CCM) na wenzake watatu ambao ni aliyekuwa Kamishna Jeneral wa Zimamoto na uokoaji, Thobias Andengenye, Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Jacob Kingu na Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhandisi Hamad Yusuph Masauni wote watahojiwa leo kwa nyakati tofauti.

Wote wanne wanahojiwa kufuatia agizo la Rais, Dk.John Magufuli kufuatia mkataba ilioingiwa na wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi wa Sh.trilioni 1.

Mwisho


Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.