JIJI LA DODOMA LAJIVUNIA KUWEZESHA WAFANYABIASHARA


Na. Dennis Gondwe, DODOMA
HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma inajivunia kutoa fursa kwa wafanyabiashara kuweza kufanya shughuli zao katika masoko yake na kukuza kipato chao na taifa kwa ujumla.
Afisa Masoko, James Yuna

Kauli hiyo ilitolewa na afisa masoko wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, James Yuna alipokuwa akiongea katika kipindi cha Dodoma ‘Live’ kinachorushwa na kituo cha redio cha Dodoma FM.

Yuna alisema kuwa Halmashauri inajivunia fursa inayotoa kwa wafanyabiashara kuweza kufanya shughuli zao katika maeneo ya masoko yaliyopangwa kwa mujibu wa taratibu. “Ndugu mtangazaji, mafanikio ni mengi katika eneo hili la masoko. Tumeweza kusajili idadi kubwa ya wafanyabiashara katika masoko yanayomilikiwa na Halmashauri ya Jiji. Kikubwa zaidi ni ukusanyaji mapato katika masoko hayo” alisema Yuna.

Halmashauri ya Jiji inaendeshwa kwa mapato yanayokusanywa kutoka katika vyanzo mbalimbali, hivyo masoko ni sehemu muhimu ya kuwezesha upatikanaji wa mapato hayo, aliongeza.

Afisa masoko huyo aliwataka wafanyabiashara hao kulipa mapato kwa mujibu wa sheria. Huduma zote zinazotolewa katika Halmashauri zinahitaji fedha ili zitekelezwe, aliongeza.

MWISHO

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.