Na. Mwandishi Wetu, ARUSHA
Polisi Mkoa wa Arusha wamewauwa watu watano wanaosadikiwa kuwa
majambazi katika eneo la Matevez Kata ya Olmot jijini Arusha ambapo
yalitokea majibizano ya risasi kati ya washukiwa hao na Jeshi la Polisi.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Kamishna msaidizi wa Polisi,
Jonathani Shana akiongea na waandishi wa habari, amesema watu hao
wananodaiwa kuwa ni majambazi walikuwa safarini kuelekea wilayani Simanjiro
mkoani Manyara kwenda kufanya tukio la ujambazi na ndipo jeshi hilo lilipopata
taarifa kutoka kwa raia wema.
Katika hatua nyingine kamanda Shama ametaja baadhi ya vitu
vilivyopatikana vinazodaiwa kuibiwa katika eneo la Olasiti ikiwemo bunduki moja
aina ya Shortgun na simu mbili ambazo tayari zimetambuliwa kuwa ni mali ya
Jackson Msangi.
Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama mkoa wa Arusha ambae
pia ni Mkuu wa Mkoa huo, Mrisho Gambo ameleezea tukio hilo kama salama za mkoa
kwa waziri mpya wa mambo ya ndani George Simbachawene.
Jackson Msangi na Nikira Msangi ni baadhi ya wahanga wa tukio la
ujambazi ambao wanalipongeza jeshi hilo kwa kufanikisha upatikanaji wa baadhi
ya mali zilizoibiwa na watu hao.
Baada ya dakika thelethini na tano za majizano ya risasi kazi
imebaki kwa wananchi kutambua miili ya watu hao iliyohifadhiwa katika hospitali
ya mkoa wa Mount Meru.
MWISHO
Comments
Post a Comment