EQUIT-T YASAIDIA KUONGEZA UFAULU DARASA LA 4 KWA 91% NCHINI


Na. Mwandishi Wetu, DODOMA 
MPANGO wa Kuinua Elimu Nchini (EQUIP-T) unaotekelezwa katika shule za msingi umetajwa kusaidia kuongeza ufaulu kwa asilimia 91 katika mtihani wa darasa la nne katika mikoa tisa iliyotekeleza mradi huo kutokana na kuimarisha stadi tatu za kujua kusoma, kuandika na kuhesabu.

Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Elimu, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Gerald Mweli ameeleza mafanikio hayo katika kikao cha wadau na wafadhili wa mradi huo walipokuwa wakifanya tathmini ya mpango huo uliotekelezwa kwa miaka sita.

Amesema katika mpango huo walimu wamefundishwa kutengeneza zana za kufundishia zinazopatikana kwenye maeneo yao na kuwataka walimu kuondokana na dhana kwamba zana za kufundishia ni lazima zinunuliwe.

Kwa upande wake Mratibu Msaidizi wa mradi huo Mwalimu Joseph Katabalo amesema program hiyo ilianzishwa katika mikoa ambayo ufaulu wake ulikuwa chini kwa miaka mitatatu mfululizo kabla ya kuanza kwa program hiyo huku Ofisa Elimu Mkoa wa Tabora, Suzana Mwalubamba akieleza mafanikio yaliyopatikana ambapo kuanzia mwaka 2014 kulikuwa na shule 700  na hadi sasa kuna shule 805 za msingi.
Mpango huo umetekelezwa kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Uingereza (DFID) kwenye mikoa ya Kigoma, Tabora, Shinyanga, Simiyu, Dodoma, Singida, Katavi, Mara na Lindi na Halmashauri 63.

MWISHO

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.