WABUNIFU NCHINI WATAKIWA KUSAJILI KAZI ZAO


Na. Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
Wabunifu nchini wametakiwa kuhakikisha wanazisajiri bunifu zao ili kuweza kuzilinda na kujipatia manufaa  katika bunifu hizo na hatimaye kukuza uchumi wa nchi na maendeleo ya jamii kwa ujumla.

Rai hiyo imetolewa jijini Dar es Salaam na afisa mtafiti kutoka kituo cha uhawilishaji wa teknolojia ambaye pia ni mtaalamu wa masuala ya haki miliki na bunifu kutoka COSTECH,  Judith Kadege ambapo amesema kuwa  Kufuatia kuwepo kwa changamoto hiyo ya kutosajiri bunifu hizo Tume ya Sayansi nchini ikaamua kuja na semina ya siku nne ya kuwajengea uwezo wabunifu wa mashindano ya kitaifa ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu (MAKISATU) ili kuweza kuwasaidia wabunifu hao  namna ya kulinda bunifu zao na kujua nyezo ambazo wanaweza kuzitumia.

Aidha, amesema kuwa kuwakutanisha wabunifu hao kutaweza kuwasaidia  kujua wapi wapeleke bunifu zao ili kuweza kufanyika kazi na pia kuwawezesha  wamiliki  uwezo wa kuongea na makumpuni makubwa kuweza kutumia teknojia za wabunifu.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa kitengo cha   uhawilishaji wa kiteknolojia Dkt. Athumani Mgumi amesema kuwa lengo la mafunzo hayo ni sehemu ya ahadi ya serikali katika kuendeleza bunifu ili kuboresha teknolojia zao.

Semina ya siku nne   ya kuwajengea uwezo wabunifu wa mashindano ya kitaifa ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu (MAKISATU) inatarajiwa kufungwa na Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia.
=30=


Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.