Vijana washauliwa kuwekeza Kilimo cha Nyanya


Na.Gibson Gabriel, TABORA

Msimamizi wa kituo cha mradi wa kilimo cha umwangiliaji katka eneo la Maili tano kilichopo Kata ya Ipuli mkoani Tabora Said Omary amewataka vijana kujiendeleza katika kilimo cha bustani ili kujikwamua kiuchumi.
Bustani ya Nyanya

Akiwa katika sehemu ya kazi, Omary amesema kuwa kilimo cha nyanya kinaweza kukuza kipato cha mtu bila kutengemea ajira kutoka serikalini. "Mfano kama aina ya Segefu one ambayo ni aina ya nyanya ambayo inakuwa kwa kupanda juu ambapo ukianza kuvuna uchukuwa miezi mitatu ukilinganisha na aina nyingine” amesema Omary.

Kwa upande mwingine Omary amefafanua kuwa aina hiyo ya nyanya hudumu kwa muda mrefu hivyo husaidia kupata faida kutokana na kutoa matunda mengi kwa muda mrefu.

Aidha, kilimo cha bustani ya nyanya kimekuwa kikisaidia kuinua kipato kutokana na kilimo hicho kuwa na bei kubwa hasa pale shamba likianza kuivisha matunda.

Kutokana na kilimo cha bustani ya nyanya kimemsaidia Omary kununua kiwanja. Aidha, amewataka vijana kutopuuzia kilimo hicho kwa sababu husaidia kubadilisha hali ya kimaisha.

Nae Martine Anthony anayefanya biashara ya nyanya amesema kilimo cha nyanya anakipenda kwa sababu humwingizia kipato kikubwa kinachomfanya kumundu  mahitaji yake ya kimaisha.

vijana wengi wamekuwa wakikataa kufanya kazi wakisubilia ajira ambazo ni ngumu katika wakati huu na kuwashauri kuodoa woga wa kuthubutu kuanzisha vitu ambavyo vitawainua kuuchumi.


Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.