TARURA SINGIDA KUPIGA FAINI WANAOKIUKA SHERIA ZA MAEGESHO


Na. Mwandishi Wetu, SINGIDA

Ofisi ya Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Wilaya ya Singida imesema itaendelea Kutoza faini kwa madereva wanawaokiuka sheria za maegesho ili kufanikisha mpango wa Serikali juu kukusanya mapato Kupitia ushuru wa maegesho yaliyo rasmi.

Akizungumza na Mtandao wa Dodoma News Ofisini kwake, Meneja wa TARURA Wilaya ya Singida, Injinia Elgidius Method amekiri kuwa zoezi la utozaji faini kwa madereva lipo na ni endelevu lengo likiwa ni kudhiti uegeshaji usio rasmi unaopelekea Serikali kupoteza mapato ya ushuru wa maegesho.

Amesema TARURA wamepewa dhamana ya kuchukua ushuru wa maegesho katika kaeneo ya maegesho. Alisisitiza kuwa utaratibu huo unafanyika pia katika Mikoa mingine ili Kuepusha madhara yanayoweza kusababishwa na uengeshaji kiholela na kurahisisha kukusanyaji wa ushuru.

Kauli ya Meneja wa TARURA Wilaya ya Singida inakuja siku chache baada ya kikao baina ya Mkuu wa Kitengo cha Usalama Barabarani Mkoani Singida na madereva wa Bajaji na Bodaboda kilichoibua sintofahamu kuhusu TARURA namna wanavyotoza faini kwa madereva. 

Mmoja wa madereva wa Bajaji mkoani Singida, Hassan Mapunda ambaye alihudhuria katika kikao hicho amesema TARURA wameenda mbali zaidi katika wajibu wao ambapo wamekuwa wakiwakamata pasipo sababu ya msingi.

Mapunda amesema TARURA wanapaswa kukutana na madereva na kuwapa maekelezo juu ya namna wanavyotakiwa kufanya badala ya kuwatoza faini bila ya kuwapa utaratibu maalumu wa kufuata.
=30=

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.