KMC Hoi Nyumbani Mbele ya Simba SC


Na. Gibson Gabriel

Klabu ya soka ya KMC ya Dar es Salaam imekubali kipigo cha magoli 2-0 kutoka kwa mabingwa watetezi Tanzania bara Simba SC katika mchezo uliopingwa katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.
Wachezaji wa Simba wakishangilia goli

Katika mchezo huo Simba walianza kujipatia goli la kwanza kupitia kwa Deo Kanda baada ya kupokea pasi murwa kutoka kwa Hasani Dirunga na kuiandikia Simba goli la kwanza.

KMC ikiwatumia viungo Kenny Ally, Batista Mgiraneza, Boniface Magaga walionekana wakijitahidi kuimudu Simba mnamo kipindi cha kwanza kitu kilichomfanya kocha wa Simba kuwatumia mawinga kuishambulia KMC kutokea pembeni.

Katika mchezo huo magoli yote ya Simba yalipatikaa kipindi cha pili kupitia kwa Deo Kanda na Gerson Fraga aliye funga goli hilo nje ya eneo la 18 katika dakika za nyongeza.

Baada ya mchezo wa KMC kupoteza imebaki katika nafasi ya 17 katika msimamo wa ligi kuu Tanzania bara ikiwa katika hatari ya kuchezea mstari wa kushuka daraja kama wataendelea kupoteza michezo.

Kuingia kwa viungo Clotus Chama na Fras Kahata kulibadilisha  sura ya mchezo ambapo waliongeza presha kwa KMC wakajikuta wakifungwa goli hizo 2-0.

Kutokana na mchezo huo KMC wamebaki nafasi ya 17 na point 9 huku wakimfanya Simba SC kuendelea kujikita kileleni akiwa na pointi 31 na michezo 12 aliyocheza ya ligi kuu Tanzania bara msimu huu.

Ikumbukwe klabu ya KMC msimu jana walimaliza katika nafasi ya nne ambayo iliwapeleka kucheza michuano ya kombe la shirikisho barani Afrika.

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.