JAPAN KUSAIDIA KUFUFUA SHIRIKA LA UVUVI TANZANIA


Na. Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM

Serikali ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania imepokea msaada wa fedha wa zaidi ya shilingi bilioni nne kutoka kwa serikali ya Japan kwa ajili ya kufufua shirika la Uvuvi Nchini –TAFICO wenye lengo la kuboresha maisha ya wananchi kiuchumi.
Kupitia msaada huo vifaa mbalimbali vitanunuliwa ikiwa ni pamoja na meli ya Uvuvi yenye vifaa vya kisasa, mashine ya kutengeneza barafu, ghala la baridi la kuhifadhi samaki pamoja na gari la lenye mitambo maalumu ya barafu na gari aina ya ‘Pickup’ kwa ajili ya kusambaza samaki.
Akizungumza katika utiliaji saini juu ya mkataba huo  Jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dotto James amesema mradi huo utaongeza  uuzaji wa samaki nje ya nchi ambapo kiwango cha ukuaji kwa shughuli ndogo zilifikia zaidi ya asilimia 9 pamoja na kuchangia pato la Taifa kwa  asilimia 1.7  kwa mwaka 2018.
Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Rashid Tamatamah ameeleza kuwa mradi huo utaisaidia sekta hiyo kufanya kazi kisasa kutokana na kununuliwa kwa vifaa mbalimbali ambapo mchakato huo ulianza tangu Januari 2018.
Kwa upande wake mkuu wa ushirikiano wa maendeleo, Ubalozi wa Japan, Shintaro Hayashi amesema  Serikali ya Japan imekuwa ikiisaidia  Serikali ya Tanzania  ambapo licha ya mkataba huo Serikali ya Japan imesaidia katika maeneo mengine  ikiwa ni pamoja na miundominu kama vile barabara, sekta ya Maji, sekta ya Kilimo pamoja na Afya.
=30=

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.