JAMII YASHAURIWA KUHAMASISHA UMUHIMU W ELIMU VIJIJINI


Na. Mwandishi Wetu, CHAMWINO
Taasisi zinazotete haki za watoto zimeombwa kutembelea maeneo ya vijijini ili kuhamasisha umuhimu wa elimu kwa wanafunzi hususani watoto wa kike.
Hatua hiyo imekuja kufuatia baadhi ya wazazi na walezi kuwaeleza watoto wao kufanya vibaya katika mitihani ya kuhitimu darasa la saba ili waweze kuwaozesha na kujipatia kipato.
Jenifa Mwombeki ni mwalimu katika shule ya msingi Nzali iliyopo wilayani Chamwino amesema wanafunzi wanahitaji kushauriwa vizuri ili kuachana ushauri wa kuwataka kufanya vibaya kwa makusudi.
Joyce ni binti mwenye ulemavu wa ngozi ni miongoni mwa wanafunzi waliomaliza darasa la saba katika shule ya msingi Nzali anasema haikuwa rahisi kumaliza kwa sababu alipitia vishawishi hivyo vya kuelezwa kufanya vibaya kwa makusudi katika mitihani ya darasa la saba.
“Nilipofika darasa la saba vilikuja vishawishi ambavyo vilikuwa vinanitisha vingine na kunifanya viongope. Lakini mimi sikusikiliza hizo sauti, wazazi wangu pamoja na wengine walikuwa wananiambia nijifelishe maana nitachaguliwa shule ya mbali. Lakini mimi sikusikia hizo sauti nikafanya vizuri matokeo yalipotoka nikawa nimepangiwa Tumaini sekondari ambayo ipo singida shule ya wasichana. Fomu ilipokuja ilikuwa na mahitaji mengi na laki nane ukiangalia na uchumi wa nyumbani ikawa inashindikana” anasema Joyce. 
Aidha, aliwashauri wazazi kuwaacha watoto wasome ili watimize ndoto zao.  
Mtandao wa Dodoma News  umezungumza na baadhi ya wazazi ambapo wamesema ili kuondokana na tatizo hizo ni lazima kuwepo kwa ushirikiano kati ya wanafunzi, walimu na wazazi.
=30=


Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.