CHANGAMOTO KIVUKO CHA MIGUU MTAA WA HAZINA



Na. Mwandishi Wetu, DODOMA
Wananchi wa Mtaa wa Hazina Jijini Dodoma waelezea changamoto wanazokumbana nazo katika kivuko cha miguu katika kipindi cha mvua.
Wakizungumza na Mtandao wa Dodoma News  wamesema kuwa wanakutana na changamoto za kupita katika eneo hilo ikiwa ni udogo wa kivuko hicho pamoja na ubora wake ukilinganisha na idadi ya watu wanaopita hapo.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Mtaa wa Hazina, Azizi Seif amesema kuwa tatizo la kivuko limekuwa changamoto na pia hakikidhi mahitaji ya watumiaji wa mtaa huo kutokana na  udogo wa kivuko hicho na kiwango kilichojengwa ukilinganisha na pesa zilizotumika.
Aidha, ameongeza kuwa mazingira ya eneo hilo ni hatarishi hasa kwa watoto kuchezea Maji machafu na kwa walemavu kupata ugumu wa   kuvuka kutoka mtaa mmoja kwenda mtaa wa pili kutafuta huduma za kijamii.
Ikumbukwe kuwa katika kipindi cha nyuma kilichopita eneo hilo lilisababisha maafa kwa Maji kumsomba mtu mmoja na mifungo mbalimbali hivyo wananchi wanaoishi pembezoni mwa eneo hilo wametakiwa kuwalinda watoto wao wasichezee Maji machafu ili kuwakinga dhidi ya magonjwa ya mlipuko.
=30=

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.