Chamwino waunda Mabaraza kupinga vitendo vya kikatili dhidi ya watoto

Na. Jackline Kuwanda, DODOMA
Afisa Mtendaji wa kijiji cha Mpwayungu wilayani Chamwino mkoani Dodoma, Seleman Kibakaya amesema kuwa katika kijiji hicho wameunda mabaraza ya watoto katika ngazi ya kata na kijiji ili kuibua haki za watoto pamoja na kupinga vitendo vya kikatili dhidi ya watoto.

Akizungumza na Dodoma news kijijini hapo, Kibakaya amesema mabaraza hayo ni muhimu kwa watoto kwani wanapoona vitendo vya kikatili vimetokea katika maeneo yao moja kwa moja huenda katika mabaraza hayo kutoa taarifa za vitendo hivyo na  hatua huchukuliwa.

Katika hatua nyingine kibakaya amesema katika kijiji hicho kumekuwa na changamoto kwani baada ya kuwa washughulikia kesi ya unyanyasaji wa mtoto ikiwemo mwanafunzi kupewa mimba baadhi ya wazazi huchukua hatua ya kuwatorosha hao hali inayoleta ugumu katika kesi hizo kwa kukosa ushahidi.

Amesema kikubwa wanachokifanya kwa upande wa wanafunzi  wa kike wamefanya jitihada kubwa na walimu za kuwafanyia uchunguzi wanafunzi wote wa kike kila mwezi kama wakibaini  mwanafunzi ameshika ujauztio hatua huchuliwa .

Mbali na hilo amesema kinachosababisha wazazi katika kijiji hicho kuwaozesha watoto wa kike katika umri mdogo ni kukosa elimu pamoja na umasikini kwani familia nyingi ni duni.

Hahivyo, ametoa wito kwa wazazi kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za nchi kwamba kama mtoto wa kike anaumri wa miaka 18 kushuka chini haruhusiwi kuozwa huku akiwataka wazazi hao kuwasomesha watoto na kuwasimamia katika maadili ili waweze kutimiza ndoto zao.

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.