*YALIYOJIRI WAKATI WA MKUTANO WA MKUU WA MKOA WA MWANZA MHE. JOHN MONGELLA NA WAANDISHI WA HABARI KUHUSU MAADHIMISHO YA SHEREHE ZA MIAKA 58 YA UHURU LEO NOVEMBA 27, 2019 JIJINI MWANZA*



# Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye maadhimisho ya sherehe za miaka 58 ya Uhuru  na Miaka 57 ya Jamhuri 

# Maadhimisho hayo yatafanyika Kitaifa Mkoani Mwanza tarehe 9 Disemba, katika Viwanja vya CCM Kirumba 

# Kauli mbiu ya Sherehe hizo ni; Miaka 58 ya Uhuru na Miaka 57 ya Jamhuri:Uzalendo, Uwajibikaji na Ubunifu ni Msingi wa Ujenzi wa Uchumi  wa Taifa "

# Sherehe hizi zinafanyika Kitaifa kwa mara ya kwanza Kanda ya Ziwa mkoani Mwanza 

#Maadhimisho yatapambwa na vikundi vya Burudani wakiwemo Wasanii wa Kizazi kipya na Ngoma za asili kutoka mikoa ya Mwanza, Kagera na Mara. 

#Baadhi ya viongozi wanaotarajiwa kuhudhuria Sherehe hizi ni pamoja na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Wawakilishi na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa 

#Viongozi wastaafu  wakiwemo Marais,Makamu wa Rais na Mawaziri wanaotarajiwa kuhudhuria 

# Wakuu wa Mikoa na Viongozi mbalimbali wa mikoa ya Kanda ya Ziwa watashiriki katika kufanikisha maandalizi ya Sherehe hizi

#Juma la kilele cha maadhimisho haya litakuwa na shughuli mbalimbali zitakazofanyika kikanda kuanzia Disemba 2, 2019 hadi tarehe 8,Disemba 8, 2019 katika mikoa ya Kagera, Mara, Geita, Simiyu, Shinyanga na Mwanza 

# Shughuli za Kikanda zilizoandaliwa na mkoa wa Mwanza ni pamoja na  Kongamano la Wanafunzi wa vyuo vya Elimu ya Juu  litakalofanyika Disemba 6, 2019 Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino Mwanza 

# Shughuli nyingine zitakazofanyika  ni pamoja na mechi ya mpira wa miguu, Mchezo wa bao, Mpira wa Kikapu, Pete na Volleball,Mashindano ya mbio za Mitumbwi, Ngonjera, Maigizo,Kwaya na Mashairi.

*Imeandaliwa na Idara ya Habari MAELEZO*


Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.