WAHITIMU CHUO CHA MIPANGO WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA


Na Jackline Victor Kuwanda, DODOMA

Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji amewataka wahitimu wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo vijijini kwenda kutumia maarifa na ujuzi walioupata wakati  wakiwa chuoni, kuchangamkia fursa zilizopo katika kujiajiri na kuzalisha ajira kwa vijana na watanzania wote kwa ujumla.

Dkt. Kijaji ameyasema hayo jijini Dodoma katika mahafali  ya 33 ya chuo hicho kampasi kuu ya Dodoma kwa mwaka 2019.
Wahitimu wa Chuo cha Mipango na Maendeleo Vijijini

Aidha, ameongeza kuwa Serikali itaendelea kuboresha mazingira ya upatikanaji wa mitaji kwa vijana kupitia bajeti za Halmashauri, benki ya maandeleo ya kilimo, asasi  za kifedha pamoja na benki za biashara nchini.


Naibu Waziri ametoa maelekezo kwa uongozi wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini kuongeza juhudi kwenye eneo la utafiti kwa sababu bila utafiti hakuna mamlaka ya kusema wala kushauri chochote mbele ya uso wa Tanzania na Dunia nzima kwa ujumla.

Kwa upande wake Mkuu wa Chuo cha Mipango Prof. Hozen Mayaya amesema chuo kimekuwa kikitoa mchango mkubwa kwa jamii ambapo watumishi kutoka zaidi ya Taasisi mia mbili  kutoka Serikali kuu, Mamlaka ya Serikali ya Mtaa, Mashirika ya Umma na taasisi binafsi wamepata mafunzo mbalimbali kwa lengo la kuongeza ufanisi kwenye  majukumu yao.

Nao wahitimu ambao wamehitimu katika chuo hicho Wamezungumza kwa furaha kwa kuhitimu kwao huku wakisema kuwa yale ambayo wameelekezwa kuyafanya huko wanako kwenda wataenda kuyafanyia kazi ikiwemo suala la kujiajiri.
=30=

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.