KONGAMANO LA CHUO CHA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE LAFANYIKA



TAASISI za elimu nchini zimetakiwa kuwaandaa wasomi kwa  kuwapa maarifa yatakayowezesha kutumia rasilimali zilizopo hapa nchini  vizuri ili kuleta maendeleo endelevu kwa ajili ya taifa.

Kauli hiyo imetolewa na Naibu  Mkuu wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere kampasi ya kivukoni jijini  Dar es Salaam, Profesa Richard Kangalawe wakati wa  kusanyiko la wasomi wahitimu wa chuo hicho.
Kusanyiko la wasomi wahitimu wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere


Profesa Kangalawe amesema nchi ya Tanzania si maskini bali wasomi wana kazi kubwa ya kufikiria kwa umakini kwa kutumia rasilimali zilizopo zilete maendeleo endelevu kwa taifa.

“Tanzania si maskini kazi kubwa ni wasomi kukuna vichwa vyetu ili kutumia rasilimali zilizoko kuleta maendeleo,” alisisitiza Prof. Kangalawe.

Alisisitiza kuwa duniani kote wahitimu wa vyuo vya elimu ya juu wamekuwa ni chachu ya maendeleo katika taasisi husika wanazozihudumia kwa kuwa wamekuwa ndio wafadhili wakubwa wa program mbalimbali za masomo  vyuoni.

Prof. Kangalawe amesema wasomi  wanahitajika kwa ajili ya kusimamia uchumi wa viwanda kwani maendeleo endelevu ni suala la ulimwengu mzima ndio sababu umoja wa mataifa ulianzisha malengo ya maendeleo endelevu ambayo yanataka dunia kuyasimamia.

Kwa upande wake Katibu wa Kamati ya kusanyiko hilo, Jumanne Muluga alisema changamoto kubwa kwa wahitimu ipo kwa kuwa bado hawajarudisha kile walichokipata kwa jamii.

Kwa upande wake  Dkt. Ahmed Sovu ambaye ni mhadhiri chuoni hapo alisema wasomi wamekuwa na mchango mkubwa katika kusaidia na kuhamasisha masuala mbalimbali kwa kutambua mazingira na kutoa masuluhisho yanayozunguka jamii.

Imetolewa na:
Kitengo Cha Habari na Mawasiliano
Chuo Cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere

PICHA ZA MATUKIO




Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.