TAKUKURU Dodoma yamshikilia Bwana Jumbe kwa kujifanya Afisa wa TAKUKURU



Na Jackline Kuwanda,Dodoma.

Mkazi wa eneo la kisasa jijini Dodoma Bwana Saimon Mapunda  Jumbe (43) anayejishughulisha na kazi  za fundi ujenzi anashikiliwa na Taasisi ya kuzua na kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoni hapa  kwa kosa la kujifanya Afisa wa Takukuru kinyume na kifungu cha 36 cha sheria ya kuzuia na kupambana Rushwa  sura 329 marejeo ya mwaka 2018.

Bwana Simon Mapunda Jumbe Mkazi wa kisasa jijini Dodoma 


Mtuhumiwa huyo amekuwa akijfanya Afisa Takukuru kwa kuwalaghai watu na kudai fedha akisingizia kwamba atawasiadia kupata ajira TAKUKURU na ofisi zingine za serikali.

Akizungumza leo na Waandishi wa habari , Mkuu wa TAKUKURU Mkoani hapa Sosthenes Kibwengo amesema kuwa uchunguzi wao umebaini kuwa mtuhumiwa amekuwa akifanya utapeli katika maeneo mengi na kutumia mbinu mbalimbali .

Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Dodoma Sosthenes  Kibwengo 


‘’ katikati ya mwezi april mwaka, tulipokea taarifa kwamba mtuhumiwa Bwana Jumbe anajiita Afisa Takukuru Mkoa wa Dodoma ,ufuatiliaji wetu umeonesha kwamba mtuhumiwa aliwaahidi kaka wa mtoa taarifa wetu kazi ya udereva ndani ya takukuru na baada ya mtu huyo kumweleza kwamba hana leseni ya udereva daraja c ndipo mtuhumiwa akataka apewa shilingi laki tatu na hamsini (350,000) ili amsaidie kupata leseni baada ya kupokea taarifa hii na sisi tukaweka mtego na kumnasa mtuhumiwa akiwa eneo la kisasa jijini Dodoma tarehe 14/4/2020’’ Alisema’’ kibwengo

Katika hatua nyingine , amesema kuwa TAKUKURU inawashikilia watu watatu kwa makosa ya kuomba na kupokea Rushwa.

‘’Takukuru Mkoa wa Dodoma inapenda kuufahamisha umma kuwa imeafikisha mahakama ya hakimu mkazi Dodoma kuwafungulia shauri la jinai Na.80/2020 watu watatu ambao ni Bwana Chizenga Masagasi Chimya (56) ambaye ni afisa mtendaji wa kijiji cha muungano wilaya ya chamwino na Bwana Salehe Wistone Chagulula (45) makosa ya kuomba na kupokea hongo ya shilingi elfu sabini pamoja na Bwana Jonas ivan Nganje (48) ambaye mwenyekiti wa kitongoji cha iyoyo naye atafikishwa mahakamani kwa kosa la kushawishi na kupokea shilingi elfu ishirini na tano (25,000) kwa mtoa taarifa ‘’ Kibwengo

Akizungumzia agizo la serikali la kufuatilia Madeni ya vyama vya ushirika ,kwa kipindi cha April ,2020, amesema TAKUKURU Dodoma imefanikiwa kurejesha shilingi milioni hamsini na saba,laki tano sitini na sita elfu miambili thelathini na mbili na senti hamsini (57,566,232.50) kutoka kwa viongozi wanachama 41 wa vyama sita vya akiba na mikopo (SACCOS) husika zinazostahili.

‘’kutokana na takwimu hizo hadi sasa Takukuru mkoa wa Dodoma tumeokoa jumla ya shilling milioni mia moja tisini na nne na wiki ijayo kwa kushirikiana na Mrajis Msaidizi wa vyama vya ushirika tukakabidhi fedha hizo kwa saccos husika zinazostahili’’ Kibwengo

Hatahivyo, amekikumbusha Chama cha walimu (CWT)  ambao wanaendelea na chaguzi zao mkoani hapa kujiepusha na vitendo vya rushwa na kwamba wataendelea kufuatilia chaguzi hizo na kuwahoji na kuwachukulia hatua stahiki wale wote wanaothibitika kujihusisha na vitendo vya rushwa bila kujali nafasi zao.

‘’cha msingi wote wanatakiwa kuzingatia mwongozo na taratibu za chama nan chi katika chaguzi hizo kujiepusha na vitendo vya rushwa hii ni pamoja na wale wote wanahojiwa na Takukuru,tunawataka mara moja tabia ya kutoa taarifa za chunguzi zetu kwani hilo ni kosa kwa mujibu wa sheria na hatua stahiki zitachukuliwa kwa wote wakatakao bainika’’ Kibwengo

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.